SITAKUSAHAU ANGEL...SEHEMU YA NNE

Admin
By -
1 minute read
0
Baada ya masaa  kadhaa kijana Steven alifika katika mpaka wa nchi  ya Zimbabwe na Afrika ya kusini ambapo alifuata taratibu zote za kuvuka mpaka kwakuwa alikuwa na nyaraka zote zinazo mruhusu kuingia Afrika ya kusini


Ndipo safari ikaendelea na hatimae saa kumi na mbili hasubui akawa amewasili Johannesburg park station

Kama ilivyo kawaida abilia wote wakashuka kwenye basi na ndugu zao waliokuja kuwapokea wakawa wamewapokea lakini ilikuwa tofauti kwa Steven maana hakuna aliye kuwa anahamiana nae kwenye nchini ya Afrika kusini


Ikabidi atoke  nje ya kitua cha basi huku akiwa hajui wapi pakwenda kwakuwa alikuwa ni mgeni na alikuwa na pesa chache kiasi cha Randi miatatu tuu wastani wa kama tsh 70000.


Baada ya kusimama saana huku akiwa hajui wapi pa kwenda ndipo akatokea RAIA mmoja wa Kenya ambae kwa haraka tu alivyomwona Steve akamjua kuwa ni mtanzania

Mkenya Huyo akamsogelea Steven huku Steven akiogopa akizani anataka kupolwa kwakuwa alishawai kuambiwa kuwa Afrika ya kusini kuna matukio mengi ya kupolwa

Mkenya alizidi kumsogelea Steven ndipo Steven akawa  anaingiwa na hofu huku akirudi nyuma mkenya akamwambia usiniogope Mimi ni RAIA mwema tuu na ajamuuluza wewe ni mtanzania..? Steve akamjibu ndiyo Mimi ni mtanzania


Ndipo nae akajitambulisha kuwa ni mkenya na unaishi hapa kwa miaka mitano sasa akamuuliza Steve he una ndugu hapa..? Steve akamjibu hapana sina ndugu nimekuja kutafuta maisha na nahitaji msaada


Mkenya yule akamjibu usiwaze Mimi nitakupeleka mtaa unaitwa Ibrow huko kuna watanzania  wengi lazma watakusaidia tuu

Baada ya maongezi machache ikaanza safari ya kuelekea ambako  alimuhaidi atapata msaada kutoka kwa watanzania wenzake….

INAENDELEA…
Mtunzi:Steve christian
0713861567
Tags:

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)
Today | 19, March 2025