Header Ads Widget

DAWA MBADALA YA KURUDISHA UKE ULIO TANUKA AU KUREGEA

Jinsi gani ya kukaza uke au ni namna gani kufanya uke uwe mdogo tena ni mada au somo lisilopendwa kuzungumzwa na watu wengi.

Ikiwa wewe ni mmoja wa waathirika na tatizo hili basi tumia muda wa kutosha kusoma makala hii sasa hivi, irudie mara nyingi mpaka umeielewa.

Kwenye makala hii nakwenda kukuonyesha baadhi ya mbinu za jinsi gani ya kurudishia tena uke mkubwa au uliolegea na kuwa mdogo tena ukiwa nyumbani bila kuhitaji kutumia matibabu mengine ya bei kubwa.

KINACHOSABABISHA UKE KULEGEA

Uke kulegea au kuwa mkubwa zaidi unaweza kutokea kutokana na sababu nyingi. Kumbuka pia kushiriki tendo la ndoa mara chache siyo suluhisho la kuwa na uke mdogo. Hakuna uhusiano wa moja kwa moja wa kuwa na uke mkubwa na kushiriki tendo la ndoa mara nyingi.

Pia hakuna uhusiano wa umri na ukubwa wa uke. Wapo wamama watu wazima wana uke mdogo pia kuna wasichana wadogo kabisa wana uke mkubwa kupitiliza.

Kama ilivyo kwa uume kwamba wanaume wana uume wenye ukubwa tofauti tofauti kadharika wanawake nao kila mwanamke ana uke wa ukubwa tofauti tofauti tofauti.

Kwa kawaida hakuna mwanaume anayependa kushiriki tendo la ndoa na mwanamke mwenye uke mkubwa. Kuna tetesi zisizo rasmi kuwa hata wanaume wanaopenda kushiriki tendo la ndoa kinyume na maumbile na wake zao huanza tabia hiyo mara baada ya kuona uke umelegea kiasi cha kutokuwa na radha tena.

Uke kulegea ni matokeo ya asili ya kuchakaa na kupanuka kwa kuta zake.

Mfano mara baada tu ya kujifungua misuli ya uke inalegea na kama hutachukua hatua mapema uke unaweza kupoteza hali ya kujibana tena na kurudi kwenye saizi yake ya awali.

Sababu kuu za uke kulegea na kuwa mkubwa ni pamoja na:

* Kuzaa mara kwa mara
* Uzito na unene uliozidi
* Kujifungua kwa upasuaji
* Kuinua vitu vizito mara kwa mara
* Mazoezi mazito ya mara kwa mara
* Misukosuko ya siku za nyuma katika nyonga
* Ukomo wa hedhi
* Maumivu sugu nyuma ya mgongo
* Kupiga chafya au kikohozi mara kwa mara
* Kufunga choo au kupata choo kigumu mara kwa mara

Mlolongo huu ni wa asili, hata hivyo kuna hatua unaweza kuzichukua na hivyo kurudishia kifaa chako katika hali ya kawaida kama msichana tena.

Baadhi ya wanawake hupendelea kufanya upasuaji maalumu ili kurudishia maumbile yao kuwa madogo jambo ambalo linaweza kuwa na athari kubwa kiafya hapo baadaye.

Zipo njia za asili unazoweza kuzifuata kukusaidia kukaza tena kifaa chako ukiwa nyumbani na kwa namna za asili bila kukuacha madhara yoyote hapo baadaye.

Ili kufanya misuli ya uke ibane unaweza kutumia njia zifuatazo. Ukiweza jaribu njia 2 mpaka 3 tofauti kwa siku kwa matokeo yenye uhakika zaidi.

Mbinu mbalimbali zinazotumika kurejesha uke mkubwa au uliolegea

1. Kula chakula sahihi

Moja kati ya njia nzuri zaidi za kupunguza ukubwa wa uke ni kula mlo sahihi ambao utasaidia kujenga afya ya misuli na kuta za uke kwa ujumla.

Kwa mjibu wa watafiti ni kuwa unatakiwa ule zaidi vyakula vyenye kuhamasisha uzalishwaji wa homoni ya estrogen vyakula kama uwatu, komamanga, ufuta, maharage ya soya na bidhaa zake, karoti, tufaa (apple), viazi vikuu (yams) nk.

Vile vile hakikisha unakula vyakula vya asili zaidi na siyo vya dukani au kwenye makopo au kwenye migahawa.

Matunda fresh yanaweza kukusaidia kuwa na harufu nzuri ukeni na kuwa na uke wenye afya. Vile vile kunywa maji mengi kila siku iendayo kwa Mungu na hivyo utakuwa na shepu nzuri ya mwili wako.

2. Jeli ya mshubiri freshi

Kutumia jeli ya mshubiri au aloe vera ni moja ya njia rahisi ya asili ya kukaza uke wako. Kutumia njia hii kwangua jeli (utomvu mweupe) wa ndani wa jani la mmea wa mshubiri ukiwa freshi na upake sehemu yote ya ndani ya uke wako mara 2 mpaka 3 kwa siku kwa wiki 3 hadi 4 na hutakawia kuona matokeo mazuri.

Matumizi ya jeli ya aloe vera kusaidia kupunguza uwezekano wa uke kulegea.

Aloe Vera ni dawa asili iliyothibitika kukaza uke kwa asili bila madhara yoyote mabaya. Ina vitamini nyingi zikiwemo vitamini A, C, folic acid, choline na madini kama zinki, magnesiamu, kalsiamu na sodiamu vyote hivi ni mhimu katika kuhamasisha kukazika kwa uke kwa ujumla.

Mmea huu wa asili hauna ugumu wowote katika matumizi yake. Tumia tu jeli kutoka katika jani freshi la mu-aloe vera na utumie vidole vyako kusambaza ndani ya uke.

Kama jeli hii ikichanganywa na mate kabla ya kupaka ukeni inaweza kutumika kama dawa bora ya kulainisha pia uke mkavu na kufanya tendo la ndoa lenye kuvutia sana.

Nina uhakika kuwa hii siyo mara yako ya kwanza kusikia kuhusu kazi hii ya mmea huu. Mshubiri unatumika katika bidhaa nyingi za vipodozi za asili.

3. Zabibubata (Gooseberry)

Zabibubata ni moja ya dawa asili nzuri zaidi katika kukaza kuta za kifaa chako. Chemsha kwenye moto zabibubata 10 mpaka 12 ndani ya maji upate kama supu hivi nzito. Kisha mimina kwenye chupa safi na utunze sehemu safi na salama.

Pakaa hiyo dawa kila siku ndani ya uke wako dakika 10 kabla ya kwenda kuoga. Hii itaongeza uwezo wa kujibana tena kwa misuli ya kifaa chako.

Kwa hakika zabibubata ndiyo moja ya dawa asili za kubana uke wako tena ambazo unatakiwa uzijaribu huku ukiongeza matunda haya kwenye chakula chako kila mara.

4. Mtindi

Njia nyingine nzuri ya kushughulika na tatizo hili ambayo nataka kukufunulia kwenye makala hii kwako wewe msomaji wangu ni matumizi ya mara kwa mara ya mtindi. Hii ni kwa sababu mtindi unao bakteria wazuri wanaohitajika ili kuuacha uke katika afya nzuri muda wote. Vile vile ukitumia mtindi kila siku ni namna nzuri ya kutibu maambukizi mbalimbali katika uke.

Kikombe kimoja kwa siku (robo lita) inatosha. Unaweza pia kuweka kijiko kidogo kimoja cha chai cha mtindi ndani ya uke wako wakati unaenda kulala na uusambaze vizuri sehemu yote ya ndani ya uke wako.

Mtindi unaweza kutumia wa nyumbani au hata ule wa dukani ni sawa.

5. Kitunguu swaumu

Kitunguu swaumu kinaweza kuwa msaada katika kutibu baadhi ya maambukizi yaliyosababishwa na fangasi. Kutumia kitunguu swaumu mara kadhaa kwa wiki inaweza kuwa njia nyingine nzuri katika kusaidia uke wako kubaki salama na wenye afya.

Vile vile kitunguu swaumu husaidia kuondoa harufu mbaya katika kifaa chako.

* Chukuwa kitunguu swaumu kimoja
* Kigawanyishe katika punje punje
* Chukua punje 3 au 4
* Menya punje moja baada ya nyingine
* Kisha vikatekate (chop) vipande vidogo vidogo sana na kisu na uache hivyo katika hewa kwa dakika 10
* Meza kama unavyomeza dawa na maji nusu lita kila unapoenda kulala.

Namna nyingine nzuri zaidi ni kuviweka ndani ya kikombe kimoja (robo lita) cha mtindi freshi koroga vizuri na unywe na hii itakusaidia kupunguza harufu mbaya ya kitunguu swaumu huku ukipata faida nyingine mhimu zilizomo kwenye mtindi.

6. Mbegu za uwatu

Chemsha maji kikombe kimoja (robo lita) kisha tumbukiza vijiko vikubwa viwili vya mbegu za uwatu ndani yake na ufunike kisha acha kwa usiku mzima mpaka asubuhi.

Asubuhi kunywa hayo maji na ule hizo mbegu pia. Fanya zoezi hili mara 3 TU kwa wiki na uenndelee na zoezi hili mpaka kifaa chako kimerudi na kuwa kidogo. Hii inasaidia pia kupunguza uzito.

Mhimu – Wanawake wajawazito au wenye saratani ya matiti wasitumie dawa hii.

7. Unga wa mbegu za embe

Unga wa mbegu za embe ni dawa nyingine nzuri unaweza kutumia kukaza misuli ya uke wako uliolegea. Ukishakula embe chukua ile kokwa yake ya ndani na uianike juani, ikikauka chukua na uisage upate unga wake.

Changanya unga huu na asali kidogo kisha pakaa ndani ya kuta na sehemu yote ya ndani ya uke kutwa mara 2 kwa majuma kadhaa na uke wako utarudi na kuwa wa kawaida.

Mbegu za embe ni chanzo kizuri cha wanga, mafuta, protini, vitamini E, nyuzinyuzi, magnesiamu, vitamini B12, asidi amino nyingi nk.

8. Vitamini E

Kwa mjibu wa utafiti kuhusu faida za vitamini E ni moja ya vitamini mhimu sana ambazo ni mhimu kwa ajili ya afya bora ya mwili. Inapendekezwa kama dawa ya kutibu kisukari na shinikizo la juu la damu wakati wa ujauzito.

Hata hivyo wanawake wengi hawafahamu ukweli kwamba vitamini E ni dawa nzuri kwa uke mkavu na kufanya kuta za uke zenye afya na nguvu kama itatumika vizuri.

Unahitaji upate mafuta ya vitamini E na uwe unaweka ukeni moja kwa moja mara 1 kwa siku mpaka utakapopata uponyaji unaouhitaji. Huwa kama kidonge hivi lakini ni mafuta na kinapasukia chenyewe ndani ya uke na kusambaa bila shida yoyote.

9. Umhimu wa kufika kileleni

Moja kati ya njia nzuri zaidi zinazoweza kupelekea uke kukaza ni kuhakikisha unafikishwa kileleni unaposhiriki tendo la ndoa.

Watafiti wamethibitisha pasipo na shaka kuwa wakati mwanamke anapokuwa anafika kileleni misuli yake ya ukeni hujikaza na kujifinya vya kutosha tendo linalofanya uke kujikaza na kuwa mdogo kwa asili.

Fanya utafiti. Kama una tatizo la kuwa na uke mkubwa kuna uwezekano mkubwa tatizo halihusiani na sababu nilizozitaja hapo juu. Kuna uwezekano mkubwa hufikishwi kileleni kwa kipindi kirefu au kwa miaka mingi tangu uanze kushiriki tendo la ndoa.

Kama mwenza wako hajuwi ni dalili zipi mwanamke huwa nazo anapofika kileleni mwambie anitafute nitamsaidia kumwelewesha.

10. Fanya mazoezi yafuatayo

KEGEL – Wakati unakojoa mkojo wa kawaida uwe unajizuia kwa sekunde 10 au 15 kisha unaendelea hivyo hivyo, yaani unakojoa kidogo unaacha kwa sekunde 10 tena unakojoa hivyo hivyo huku unapumzika mpaka unamalaiza.

Fanya zoezi hili mara 3 mpaka 4 kwa siku ukienda kupata haja ndogo. Zoezi hili kwa mjibu wa watafiti ni kuwa linasaidia kukaza misuli ya uke.

SQUATS – Hili ni zoezi lingine zuri la kubana uke uliolegea. Ni kusimama na kuchuchumaa, kuchuchumaa na kusimama hivyo hivyo mara 15 kwa mizunguko mitano mara 2 kila siku. Zoezi hili linasaidia pia kuwa na maungo mazuri na faida nyingine nzuri za kiafya.

LEGS UP – Lala chali kisha nyanyua mguu mmoja juu kisha shusha chini na unyanyuwe mguu mwingine juu na ushushe chini hivyo hivyo mguu mmoja juu kisha chini, kisha mwingine juu chini ukichoka unapumzika kisha unaendelea hivyo hivyo kila siku kwa dakika 15 mpaka 20 mpaka kifaa chako kitapokuwa sawa.

Mambo mengine mhimu ya kuzingatia:

*Kuwa msafi kila mara
* Vaa nguo za ndani zinazotengenezwa kwa pamba
* Usitumie pafyumu zenye kemikali

Njia hizi nilizozielezea hapo juu zote ni nzuri katika kurejesha katika saizi ndogo uke ulikokwisha kuwa mkubwa au uliolegea. Chakula na mazoezi pia ni mhimu kuzingatia kwa matokeo mazuri na yenye uhakika.

Wakati mwingine unaweza kuchelewa kuona mabadiliko lakini usikate tama mpaka umefanikiwa. Kwahiyo kama wewe ni mmoja wa watu wamekuwa wakisumbuliwa na tatizo hili usiichukulie poa hii makala jaribu yaliyopendekezwa humu na uniletee mrejesho.

Ikiwa utahitaji dozi kamili ya dawa hizi basi niachie tu ujumbe WhatsApp +255769142586 muda wowote mimi nitakujibu.

Kuna dawa nyingine tofauti na hizi umewahi kutumia na zikakusaidia? Kama ndiyo nitajie hapo chini kwenye comment kwa faida ya wengine.

Tafadhali SHARE post hii kwa ajili ya uwapendao


Post a Comment

3 Comments

  1. Kutana na mtaalamu wa mitishamba toka tanga anatibu ugumba.. uzazi kuzaa watoto mapacha..uti sugu ..kukuza shape na hips..kubana uke ...tafadhali wasiliana na dr mkuu 0744903557 tanga

    ReplyDelete
  2. Kukuza uume na kurefusha 0744903557 tanga

    ReplyDelete
  3. Zabibubata zinazohitajika kutumika hapo ni zile kavu au mbichi??

    ReplyDelete