waziri wa afya Ummy mwalimu asema deni la taifa nje ya nchi lililotokana na matibabu lafikia bilioni 34
akiongea na wana habari amesema serikali imekuwa ikitoa garama nyingi kugharamia watu kwenda kutibiwa nje wakati matatizo hayo nchini yanatibika
amesema pia ni marufuku kwa hospitali ya muhimbili kuruhusu mtu akatibiwe nje kama ugonjwa alionao waweza kutibika nchini
pia kasema kwa wale wenye pesa zao wapo ruksa kwenda ila hii ni kwa wanao tibiwa kwa pesa za serikali
amesema Tanzania imesomesha madaktari wengi sasa ni muda muhafaka kuwatumia katika kupunguza gharama zisizo za lazima
deni hilo ni la miaka minne iliyopita na kwasasa hawaitaji kulikuza tena deni hilo bila ya sababu
Tags
afya