WATU KADHAA WAJERUIWA MSIKITINI UFARANSA

Watu kadhaa wamejeruhiwa baada ya watu kushambulia kwa bunduki waumini waliokuwa wakitoka msikitini

tukio hilo limetokea kusini mwa ufaransa katika msikiti wa Arrahma ambapo watu wawili wakiwa na bunduki mkononi walivamia watu waliokuwa wakitoka katika ibada ya jioni

watu wanne wa familia moja walishambuliwa kwa risasi akiwemo mtoto mdogo wa kike wa umri wa miaka saba alijeruhiwa

mpaka sasa majeruhi nane wapo hospitali wakipatiwa matibabu huku walio sababisha tukio hilo wakiwa hawajakamatwa mpaka sasa

polisi imesema tukio hilo si la kigaidi ni tukio tu lenye kuonesha chuki za kidini na polisi wanaendelea na uchunguzi ili wawakamate waliofanya tukio hilo

kwa mujibu wa mashuhuda walisema watu walianza kukimbia baada ya kuwaona watu wawili wakishuka kutoka kwenye gari wakiwa na bunduki mkononi ambapo mpaka sasa hakuna taarifa kuhusu vifo vyovyote


Post a Comment

Previous Post Next Post