CHADEMA WANAOTAKA KUHAMA ARUSHA WAHAME KABISA

Hivi karibuni kumekuwa na wimbi la wanachama na madiwani mkoani arusha ambao wanatangaza kuhama chama cha demokrasia na maendeleo chadema na kuhamia cccm

mwenyekiti wa chadema mkoa wa Arusha Aman golugwe amesema wanao tamani kuhama wahame mapema wasichelewe kwa kuwa wanafaham kuna wengine wapo wanampango wa kuhama kutoka katika chama hicho

miongoni mwa madiwani walio hama kutoka chadema mkoani arusha ni pamoja na Credo kifukwe kata ya mutiet,Anderson sikawe kata ya legaluki, Emanuel.moleli kata ya makiba , Greyson isagya kata ya maroron na Josephine mshiu wa viti maalum

mwenyekiti amesema wengi wanahama na hawaathiri chochote katika chama na wenye mpango wa kuhama wahame

pia mbunge wa Arusha mjinj Godbless lema alisema wengi wanao hama wanahama kwa uroho wa madaraka na ushawishi wa fedha kauli iliyo kanushwa na madiwani hao

katika mwaka wa uchaguzi mkoani arusha mwaka wa 2015  ulikuwa mzuri kwao kwakuwa waliweza kushinda majimbo sita kati ya saba na kuchukuwa kata tano kati ya saba na kuunda halmashauri.


Post a Comment

Previous Post Next Post