
Wanawake wanne wamechomwa moto na kikosi cha sungusungu katika kijiji cha Undomo wilayani nzega mkoani tabora
kamanda wa polisi amesema wanawake hao walichomwa moto mpaka kufa huku mmoja wao akipigwa kipigo kizito
amewataja marehemu kuwa ni
"ester kaswahili,Njungu maswani,Christina said na kabula kageto "
kwa mujibu wa tetesi wanawake hao wamechomwa moto wakituhumiwa kuwa ni wachawi na huwaroga watu hapo kijijini kwa kipindi kirefu
mpaka sasa polisi imewakamata diwani wa kata na mtendaji kwakuwa walikuwa wakijua kuhusu mpango wa tukio hilo lakini hawakutoa taarifa mapema
pia sungusungu walio husika wanatafutwa na polisi imepiga marufuku vikundi hivyo vya ulinzi kwakuwa vimekuwa vikikiuka maadili
Tags
Kitaifa