
Siku ya tarehe 23 mwezi july mtoto mdogo aliwa na fisi wakati akisubiri chakula cha jioni nyumbani kwao
Tukio hili limetokea katika kijiji cha Izizimba mkoani mwanza ambapo mtoto wa miaka minne aliye fahamika kwa jina la Limi Bunzama ameliwa na fisi karibu na nyumbani kwao
mtoto huyo alikuwa akicheza nje ya nyumba yao akisubiri chakula ghafla akaja fisi huyo na kumbeba kisha kwenda nae polini
baada ya muda mama wa mtoto akashtuka ndipo akaanza kumsaka akisaidiana na wanakijiji ndipo wakamkuta akiwa ameliwa sehemu kubwa ya mwili wake huku fisi akiwa ametoweka
baada ya tukio hilo wanakijiji waliamua kuanza kumtafuta fisi huyo lakini mpaka sasa hawajafanikiwa kumpata huku mtoto akiwa amesha fariki
Tags
Kitaifa