RAISI MAGUFURI AFANYA UTEUZI MWINGINE

Admin
By -
0 minute read
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Bi. Janeth Masaburi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Mhe. Rais Magufuli amefanya uteuzi huo kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayompa mamlaka ya kuteua wabunge 10 watakaokuwa miongoni mwa Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Bi. Janeth Masaburi ataapishwa kulingana na taratibu za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam



Tags:

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)
Today | 19, March 2025