Watu 30 wajeruhiwa baada ya kugongwa na gari ujerumani

Watu kadhaa wamejeruhiwa baada ya mtu aliyekuwa akiendesha gari kuuvamia umati wa watu waliokuwa wakisherehekea tamasha la Carnival Ujerumani. Polisi wamemkamata mshukiwa na wamesema ni tukio la makususdi.
Watu 30 wamejeruhiwa hapo jana ikiwa ni pamoja na watoto katika mji mdogo wa Volkmarsen magharibi mwa Ujerumani, baada ya raia wa Kijerumani aliyekuwa ndani ya gari kulivamia gwaride la watu waliokuwa wakisherehekea tamasha la kitamaduni la 'Karnival'.
"Alikuwa akiliendesha gari kwa kasi kuelekea kwenye umati wa watu. Hisia yangu ni kwamba alikuwa akiongeza kasi. Kulikuwa na sekunde chache za ukimya halafu kila mtu akaanza kupiga kelele," amesema Friedhelm Engelmann, mmoja wa wakazi walioshuhudia tukio hilo.
Waendesha mashtaka wa Ujerumani pamoja na polisi wamesema mshukiwa huyo, kijana mwenye umri wa miaka 29, amekamatwa kwa tuhuma za kujaribu kuua. Wameongeza kwamba sababu bado haijulikani, lakini tukio hilo linazingatiwa kuwa ni la makusudi huku uchunguzi ukiwa unaendelea.
"Hatufikiri kuwa hili lilikuwa ni shambulio la kigaidi. Lakini linaweza kuzingatiwa kama shambulio la makusudi. Bado hatujui sababu zake. Mahojiano ya hadi sasa hayatoshi kuweza kusema chochote kuhusu nia ya shambulio hili," ameeleza msemaji wa polisi wa jimbo la Hesse, Henning Hinn.

Post a Comment

Previous Post Next Post