BARCELONA YAIHENYESHA REAL MADRID


Image result for PICHA YA YA WACHEZAJI WA BARCELONAKlabu ya Barcelona wamewaduwaza wenyeji na watani wao wa jadi Real Madrid kwa kuwafunga mabao matatu bila jibu, katika mechi ya ligi ya Uhispania - La Liga iliyochezwa katika uwanja wa Santiago Bernabeu. 
Luis Suarez alipatia Barcelona bao la kwanza mnamo dakika ya 54 naye Lionel Messi akapachika bao la pili kwa njia ya mkwaju wa penalti, baada ya Dani Carvajal wa Real madrid kuoneshwa kadi nyekundu kwa kuzuia mpira langoni akitumia mkono.
 Bao la tatu lilitiwa kimiani na Aleix Vidal. 
Ushindi huo unaiweka Barcelona pointi 14 mbele ya Real madrid.

Post a Comment

Previous Post Next Post