Header Ads Widget

Babu Tale kumfanya dogo Janja aimbe,mwenyewe amesapoti hilo.


Meneja wa Tip Top connection ambaye pia ana mmeneji Dogo Janja amesema muda wowote kuanzia sasa msanii huyo atasikika akiwa anaimba tofauti na staili yake ya kurap ambayo wengi wameizoea.
Meneja huyo amesema kuwa yeye ni mfanyabiashara na anatoa vitu ambavyo vinahitajika sokoni ambapo anaamini kwa sasa muziki wa kuimba na kuchezeka ndio uko sokoni huku akitolea mfano wasanii wa Hip Hop waliobadilika wakiwemo wakina Madee,Professor Jay na kimbunga.
madee alikuwa ana rap,lakini alipotoka na pombe yangu ikawa ndo nyimbo iliyomuingizia myimbo kuliko zote,ikamfanya ahamie nyumbani kwake..anytime Janja anaimba,humu kagusia goma lingine anaimba yote” alifunguka Babu Tale wakati anatambulisha wimbo mpya wa Dogo Janja kwenye redio moja.
Kwa upande wake Dogo Janja alionekana akisapoti hilo kwa kusema,”siku hizi hatuokoi Hip Hop,tunaokoa maisha
Source: Clouds

Post a Comment

0 Comments