MKE AMCHINJA MUME WAKE MKOANI SHINYANGA

Mwanamke aliye fahamika kwa jina la zena mohamed (29) anashikiliwa.na polisi baada ya kumuuwa kwa kisu.mume wake aliye tambulika kwa jina la bakar salehe(35)

tukio hili limetokea kwenye mtaa wa malange mkoani shinyanga siku ya jana tarehe 20.septemba 2017 majira ya saa mbili usiku

akiongea na wana habari mkuu wa polisi amesibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akisema ugomvi huo ulikuwa ni wa wivu wa mapenzi

kwa mujibu wa maelezo mwanamke huyo alipokea simu ya mume wake na kusikia sauti ya mwanamke hatua iliyo mfanya kuhisi kuwa ni hawala wa mume wake

kufuatia hatua hii ulizuka ugomvi na hatimae jioni mwanamke huyo alimvizia mume wake akiwa amelala ndipo akamjerui na kisu mpaka kufa

baada ya kufanya tukio hilo mwanamke huyo alifungua sauti kubwa ya redio kisha kufunga mlango na kukimbilia shinyanga mjini kwa mama yake

baada ya kufika huku akiwa amechanganyikiwa akamwambia mama yake kuwa amesababisha mauaji ndipo mama yake akapiga simu polisi na kutoa taarifa na hatimae mwanamke huyo kukamatwa.

Post a Comment

Previous Post Next Post