MTOTO WA MIAKA 11 ABAKWA KISHA KUNYONGWA



Mtoto mmoja wa miaka kumi na moja mjini dar es salaam adaiwa kubakwa kisha kunyongwa

mtoto huyo wa miaka kumi na moja amekutwa amefariki kwenye kitanzi nyumbani kwao huku akiwa amesha fariki

mama wa mtoto huyo alisema kuwa alimwacha nyumbani mwanae alikuwa na mjomba wake yaani kaka wa mama wa marehemu ambae ni baba mmoja na yeye

baada ya muda akapigiwa simu kuwa mtoto wake amefariki ndipo akaenda hospital ambako mwili wa mwanae upo na alipo funua akagundua ni mwanae

baada ya kuutambua nesi alimwambia amtazame sehemu za siri maana ni kama amebakwa kutokana na michubuko aliyonayo lakini alishindwa kutazama kutokana na uchungu

mpaka sasa mjomba huyo aliye baki na mtoto amesha kamatwa na polisi ambapo kwa maelezo yake ni kwamba mtoto huyo atakuwa amejinyonga mwenyewe maana hicho kitanzi yeye alimtegea paka ambae huwa anaiba hapo kwao na haja husika katika tukio la mtoto huyo


Post a Comment

Previous Post Next Post