MLINZI JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA

Admin
By -
0

Mahakama wilayani mlele imemuhukumu miaka 30 jela mlinzi aliye fahamika kwa jina la george sikoki baada ya kumbaka binti wa miaka 16

akisomewa mashitaka na hakimu mkazi Teotimus swai mtuhumiwa alitenda kosa holi january 27 mwaka huu majira ya saa 7 usiku
wakati wazazi wa binti huyo wakiwa safarini

siku ya tukio mtuhumiwa alivunja mlango na kuingia ndani kisha kumbaka binti huyo huku akimtishia kuwa akitoa taarifa kwa watu ata muua

baada ya kufanyiwa tukio hilo binti huyo alijivuta mpaka nyumba ya jirani na na kutoa taarifa huku akivuja damu sehemu za siri baada ya kubakwa

ndipo majirani wakampeleka polisi binti huyo na kufanyiwa matibabu ambapo katika kesi hiyo mtuhumiwa alikiri kutenda kosa hilo kwa maandishi lakini alipofika mahakamani alikana mashtaka yake

mahakama kupitia mashahidi watano akiwemo dokta iye mfanyia vipimo ilijilizisha na kumhukumu mlinzi huyo kifungo cha miaka 30 jela.


Tags:

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)