AKAMATWA AKITAPELI WATU AKITUMIA SARE ZA JWTZ

Admin
By -
0
Polisi mjini tabora inamshikilia fransics kilao (31) mkazi wa kitangani shinyanga kwa kukutwa na sare za jeshi la JWTZ

akiongea na waandishi wa habari kamanda wilbord mtafungwa amesema mtu huyo anashikiliwa na polisi kwa kukutwa na vifaa vya jeshi anavyo tumia kutapeli

mtuhumiwa huyo alikamatwa JM hoteli mjinj tabora akiwa na buti,sare,kofia,sweta pamoja na mikanda mitatu ya jeshi

pia mtuhumiwa huyo amekutwa na form za kujiunga na jeshi la kilujenga taifa.JKT,barua za maombi ya kujiunga na JKT pamoja na baadhi ya nakala za vyeti vya sekondari

pia amesema mtu huyo amekutwa na mihuri ya JKT pamoja na gari aina ya toyota staret T633ARF

polisi inaendelea na uchunguzi kubaini uhalali wa gari hilo pia wapo kwenye uchunguzi pia kujua aliko pata sare hizo za JWTZ
Tags:

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)