SITAKUSAHAU ANGEL....SEHEMU YA TANO

Admin
By -
0

Ikaanza safari ya kwenda ambako atakutana na watanzania ambao  wataweza kumpa msaada akiwa ametanguzana na yule mkenya aliye kutana nae kwenye kituo cha basi

Baada ya kutembea mwendo wa kama nusu saa  kwa mguu yule mkenya akamwambia Steve "nisubiri hapa napenda kununua vocha nimpigie jamaaa atufuate"


Yule mkenya alipoaga anaenda kununua vocha huku Steve akiwa anamsubili yule mkenya akawa ameenda jumla hakuweza kurudi tena Steve akasubili saana akajikuta amebaki njia panda asijue wapi pa kwenda


Baada ya muda wa kama saa  zima akatokea mtu mmoja akamuuliza Steve "why are you here?" Steve akamjibu "I'm waiting for my friend" yule mtu  akamuuliza tena "where are you coming from?" Steve akamjibu iam from Tanzania "


Yule mtu  akamuuliza kwa kiswahili kumbe na yeye ni mtanzania akamuuliza rafiki yako ni nani? Steven akajibu ni RAIA mmoja wa Kenya aliniambia atanileta kwa watanzania watanipa msaada Mimi sina ndugu nimekuja kutafuta maisha


Yule mtu  akacheka saana akamwambia huyo  mkenya alishindwa kukwambia kuwa ameshakuleta kwa watanzania wenzako ni pamoja na Mimi

Baada ya hapo akamwambia karibu dogo  hii ndiyo Afrika kusini Kwani umeshaibiwa? Steve akauliza kuibiwa nini?akamjibu huku mgeni mala nyingi lazma aibiwe kama hujaibiwa una bahati...

Yula mtanzania akamchukuwa Steven mpaka nyumbani kwake  maeneo ya FOX STREET akampatia chakula na kumwambia  karibu dogo hapa ndiyo ghetto utaishi  hapa kwa sasa

Baada ya kumaliza kula akamuuliza Steve umeamua kuja huku umejipangaje..? Steve akauliza kujipanga kivipi? Akamjibu yaani una ujuzi wowote..? Steve akamjibu Mimi ni fundi  magari mzuri  nikipata kazi unafanya


Yule mtanzania akamjibu Steve hongera umekuja huku una fani  itakusaidia Mimi nilikuja huku sikuwa na fani nikaishia kuuza madawa ya kulevya na mpaka sasa nauza ila sitamani na wewe uingie huku ntakupeleka


INAENDELEA...

Tags:

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)