MANALA ATOA KAULI HII KWA SIMBA




Mashabiki hao wamenuna kutokana na kuishuhudia timu yao ikilitema taji la FA ililokuwa ikilishikilia tangu Mei, mwaka jana, kisha kufurushwa mapema katika Kombe la Mapinduzi.
SIMBA asubuhi ya jana imelikimbia Jiji la Dar es Salaam na kujichimbia Morogoro kuweka kambi ya maandalizi ya mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Singida United, lakini huku mashabiki wake wamenuna.

Mashabiki hao wamenuna kutokana na kuishuhudia timu yao ikilitema taji la FA ililokuwa ikilishikilia tangu Mei, mwaka jana, kisha kufurushwa mapema katika Kombe la Mapinduzi.

Kinachowatia hofu zaidi ni sintofahamu ya wachezaji na benchi la ufundi kwa jinsi walivyochuniana Uwanja wa Amaan, Unguja na hata walipotua jijini kutoka visiwani, lakini kumbe Kocha Masudi Djuma, ameshtukia mchezo.

Djuma amenong’onezwa namna mashabiki wa klabu hiyo walivyopaniki na kisha kwa kujiamini akatamka; ‘Wana Simba watulie, mambo mazuri yanakuja’.


Post a Comment

Previous Post Next Post