
Katika hali isiyo ya kawaida Panya, mende, na wadudu wengine wamefanya uharibifu mkuwa kwa kuvunja vitu vingi katika ikulu ya Marekani Ripoti zinaeleza
Vyoo miongoni mwa vitu vingi vilivyoripotiwa kwa wafanyikazi wa kufanya marekebisho katika ikulu hiyo ya Whitehouse jijin Washington DC.
Ripoti ya vitu vinavyofaa kurekebishwa katika ikulu ya White house iliopatikana na chombo cha habari cha NBC Washington ilishirikisha ripoti nyengine ya mwaka uliopita kutoka kwa utawala wa rais Obama.
Panya wanadaiwa kuonekana katika chumba cha kulia cha maafisa wa jeshi la wanamaji.
Walionekana katika majengo, kulingana na Brian Miller, aliyekuwa inspekta jenerali wa kikosi cha huduma za jumla ambacho husimamia marekebisho katika jumba hilo la rais.
''Mtu yeyote kati yetu ambaye anamiliki nyumba ya zamani anajua kwamba inahitaji kazi nyingi''.
Mende walikuwa tatizo katika chumba cha kulia huku wadudu wakionekana katika nyumba anayoishi afisa mkuu wa jeshi kulingana na ripoti hiyo.
Wadudu na mende pia walionekana katika chumba cha wanahabari.
Mbali na kukabiliana na wadudu ,ripoti hiyo ya marekebisho ya Ikulu inaonyesha kazi nyingi zilizohitajika kufanyika baada ya utawala mpya kuingia mwanzoni mwa mwaka huu.
Tags
vtuko