POLISI BADO WANAMSHIKILIA HALIMA MDEE

Mbunge wa kawe Hala mdee alikamatwa jana na polisi baada ya kuoata amri kutoka kwa mkuu wa wilaya ya kinondoni

Mdee alikamatwa jana akiwa nyumbani kwake makongo juu na kupelekwa kituo cha polisi oysterbay baada ya mkuu wa wilaya kutaka akamatwe

Mkuu wawilaya alimtaka mkuu wa polisi kinondoni amkamate mbunge huyo kwa kile alicho kiita lugha ya uchochezi iliyoyolewa na mbunge huyo alipoongea na wana habari

katika mkutano huo Halima mdee aliwataka chadema katika halmashauli wanazo zishikilia kuwarudisha  shule mabinti waliopata ujauzito kwa kuwa ni haki yao kupata elimu

kufuatia kauli hiyo mkuu wa wilaya ya kinondoni aliamuru polisi wamkamate kwakile alicho kiita lugha ya uchochezi  iliyo tolewa na mbunge huyo

Post a Comment

Previous Post Next Post