Header Ads Widget

WACHIMBA MADINI 7 WASIBITIKA KUFARIKI WENGINE HAWAJULIKANI WALIKO


 Washukiwa saba wachimba haramu wa madini walithibitishwa kufariki dunia na wengine zaidi ya 20 hawajulikani waliko na kudhaniwa wamekufa baada ya mvua kubwa kusababisha maporomoko ya ardhi.

Washukiwa saba wachimba haramu wa madini walithibitishwa kufariki dunia na wengine zaidi ya 20 hawajulikani waliko na kudhaniwa wamekufa baada ya mvua kubwa kusababisha maporomoko ya ardhi yaliyowafukia ndani ya mahandaki waliyokuwa wakichimba kwenye mgodi wa shaba nchini Zambia, polisi na mamlaka nchini humo walisema Jumamosi.

Polisi walitoa majina au baadhi ya majina ya waathirika saba waliothibitishwa na kusema wachimba migodi wote kwenye mahandaki wanashukiwa kufariki. Polisi hawakusema ni wachimbaji wangapi kwa jumla walikuwa kwenye mahandaki lakini Mkuu wa Wilaya ya Chingola Raphael Chumupi aliambia Associated Press kwamba kulikuwa na takriban watu 36.

Maafisa wa serikali walisema kuwa zaidi ya wachimba migodi 30 walikwama kwenye mahandaki lakini hawakuweza kutaja idadi kamili.

Post a Comment

0 Comments