Kupata pesa nyingi ama utajiri wa haraka huwa matamanio ya watu wengi . Walakini kunao watu ambao kiasi kikubwa cha fedha nusura kiingie mifukoni mwao lakini hawakuzipata kwa kuzikataa wakitaka kupewa zaidi au bahati haikutengenea.
Hii hapa orodha yawatu ambao wamezinusia pesa hizo lakini hazikuwafikia .Aliyetukumbusha hili maajuzi ni raia wa Afrika Kusini Nkosana Makate ambaye alivumbua huduma ya 'please call me' iliyotumiwa na kampuni ya mawasiliano ya Vodacom .
Nkosana alidai mwaka wa 2016 kwamba uvumbuzi wake uliipa Vodacom dola bilioni 5 na yeye anataka asilimia 15 ya fedha hizo .
Nkosana Makate (Shilingi Milioni 354)
Nkosana Makate, mwanzilishi wa huduma ya simu, 'Tafadhali Nipigie simu' anadai jumla ya Sh75 bilioni kama fidia kutoka kwa kampuni ya Vodacom.
Kampuni ya Vodacom mwanzoni ilikuwa imekubali kulipa Makate Sh354 milioni ambayo alikataa. Mzozo wa kampuni hiyo na mvumbuzi Makate upo kortini .
Huduma ya 'Tafadhali Nipigie' ililetwa sokoni kwa mara ya kwanza mnamo 2001. Hii ni huduma ya sms ya bure ambayo inaruhusu wateja kutuma ujumbe kwa mtumiaji mwingine anayeomba apigiwe simu.
Tags
habari