SIMULIZI SAFARI YANGU YA AFRIKA KUSINI SEHEMU YA 13

Nikamuuliza nimekuuzi kwa kitu gani? Akajibu nipo bize nitakueleza baadae nitakuambia umeniuzi kitu gani

Nikabaki nawaza Ni Nini kilichomuuzi? Nikawa sipati majibu jioni mida yaa saa kumi akanipigia akaniuliza Yale madawa ndani mwako unauza au wewe mtumiaji? Duh nilishituka nikabaki sijui nimjibu nini

Nikamwambia madawa gani? Au umeona unga wa ugari? Akajibu unanifanya Mimi mtoto? Mimi nayajua madawa usinizuge nijibu Tena Ni cocaine nimeiona niambie ukweli Mimi nijue

Nikamjibu baadae uje nikuambie ukweli nipomuambia hivo akaelewa  akasema saambil usiku nakuja na staki unifiche kitu chochote nikamjibu sawa

Kweli muda ulipofika akaja akanipikia chakula akaandaa tukala tukakaa sebureni akaniambia Sasa niambie ukweli ikabidi tu nimueleze hali halisi iliyopelekea Mimi kuingia kwenye biashara ya madawa ya kulevya... ITAENDELEA

Post a Comment

Previous Post Next Post