Kizaazaa: wajeruhiwa wakikwepa haja ndogo

Admin
By -
0
Daraja la Jannowitz
Mtu mmoja aliyejisaidi akiwa kwenye daraja mjini Berlin azua kizaazaa baada ya kusababisha watu kujeruhiwa, kwa mujibu wa idara ya zima moto mjini humo.
Mtu huyo ambaye hakujulikana alijisaidia haja ndogo kwenye eneo la mteremko wa daraja la Jannowitz kisha mkojo ukatiririka mpaka kwenye boti iliyokuwa imebeba watalii ikipita chini ya daraja.
Watu kadhaa waliokuwa kwenye boti hiyo waliruka ghafla, wakajigonga vichwa vyao wakati boti ilipokuwa inapita chini ya daraja.





Watu wanne walipelekwa hospitali kwa gari la kubeba wagonjwa wakiwa na mikwaruzo kichwani.
Haijajulikana kama mtu huyo alitozwa faini au alikamatwa.
Kitendo cha mtu huyo kilikosolewa kwenye mitandao ya kijamii.
Mtu mmoja aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter: ''Wanyama kwenye bustani yao wana tabia njema.''



























































































































































































































































































































































































Tags:

Post a Comment

0Comments

Post a Comment (0)